MATANGAZO YA USHARIKA

                                LEO TAREHE 28 NOVEMBA, 2021

                         NENO LINALOTUONGOZA SIKU YA LEO NI 

                              BWANA ANALIJIA KANISA LAKE.

1. Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli. 

2. Wageni: Hakuna wageni waliotufikia na vyeti.

3. Matoleo ya Tarehe 21/11/2021

Tunamshukuru Mungu aliyetupa afya ya kumwabudu na utayari wa kumtolea kwa hiari mali alizotupa kwa kazi yake.

    NAMBA YA SADAKA KWA NJIA YA MTANDAO:

0757 391174 - KKKT AZANIA FRONT

Namba ya Wakala M-PESA – 5795794 – KKKT AZANIA FRONT CATHEDRAL

5. Tunapenda kuwakumbusha na kuwakaribisha wote katika vipindi vya kujifunza neno la Mungu hapa Usharikani kila siku za juma. Morning Glory saa 12.00 asubuhi ili kuanza siku kwa Uongozi wa Mungu, Ibada za mchana saa 7.00 -7.30 mchana tunapopata faragha binafsi na Mungu pamoja na Alhamisi Maombi na Maombezi saa 11.30 jioni. Vipindi vyote vinarushwa Mubashara kupitia Azania Front TV. Karibu

6. Leo tutashiriki chakula cha Bwana. Washarika tujiandae.   

7. Jumapili ijayo tarehe 05/12/2021 tutamtolea Mungu fungu la kumi. Aidha siku hiyo ibada itakuwa ni moja itakayoanza saa 1.00 asubuhi, ikiambatana Mkutano Mkuu wa Usharika. Washarika tuiombee siku hiyo.

8. Uongozi wa Umoja wa Vijana unapenda kuwatangazia Vijana wote kuwa kutakuwa na semina tarehe 09/12/2021 kuanzia saa 2 asubuhi. Hivyo wanaomba vijana waliotayari wajiandikishe majina yao kwa uongozi wa Umoja wa Vijana kwa ajili ya Maandalizi. Sehemu itakapofanyika semina vijana watajulishwa.

9. Wazazi na Walezi wenye watoto wanaoanza Kipaimara mwaka wa Kwanza 2022 wafike Ofisi ya Parish Worker ili wajiandikishe. Umri ni kuanzia miaka 12 na kuendelea.

10. IBADA ZA NYUMBA KWA NYUMBA

- Mjini Kati: Kwa njia ya Mtandao

Makumbusho, Kijitonyama, Sinza, Mwenge, Makongo na Ubungo: Mama Mamkwe.

11. NDOA.

NDOA ZA WASHARIKA

KWA MARA YA KWANZA TUNATANGAZA NDOA ZA TAREHE 18/12/2021 

SAA 8.00 MCHANA

Bw. Emmanuel Melckizedeck Sanare na Bi. Agatha Silas Kaaya

KWA MARA YA TATU TUNATANGAZA NDOA ZA TAREHE 04/12/2021 

SAA 10.00 JIONI

Bw. Emmanuel Benson Jonas na Bi. Florida Renatus Kyando

NDOA IFUATAYO ITAFUNGWA USHARIKA WA GEZAULOLE DAYOSISI YA KASKAZINI KATI YA

Bw. Anold Weransari Kimambo na Bi. Aikande Elisante Lema

VILE VILE NDOA IFUATAYO ITAFUNGWA CCT CHAPLAINCY CHUO KIKUU UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM

Bw. Mulashani Emanzi Bikombo na Bi. Anna Emmanuel Mbijima

Matangazo mengine ya Ndoa yamebandikwa kwenye ubao wa matangazo karibu na duka letu la vitabu.

11. Zamu: Zamu za wazee leo ni Kundi la Kwanza

Na huu ndio mwisho wa matangazo yetu, Mungu ayabariki.