MATANGAZO YA USHARIKA

TAREHE 14 MEI, 2017

NENO LINALOTUONGOZA SIKU YA LEO NI MWIMBIENI BWANA WIMBO MPYA

  1. Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli.
  1. Wageni: Hakuna Wageni waliotufikia na cheti.
  2. Leo hatutakuwa na Kipindi cha maombi na maombezi. Aidha siku ya alhamisi tarehe 18.05/2017 saa 11.30 jioni kutakuwa na kipindi cha maombi na maombezi. Atakayeongoza ni mtumishi Emmanuel Shemdoe.Wote mnakaribishwa.
  3. Washarika wanaoishi Oystabay na Masaki wanaombwa kukutana chini ya mti hapo nje mara baada ya ibada hii.

Neno: Zaburi 121, Wimbo: Wakisukuma (Wataimba wanandugu)

4. Jumapili ijayo tarehe 21.05.2017 baada ya ibada ya pili, wanaume wote wa Usharika wa Azania Front Cathedral wanaombwa kukutana kwa ajili ya kupokea taarifa ya Kamati ndogo  iliyoteuliwa na mkutano Mkuu waUsharika kupendekeza jinsi ya kuanzisha Umoja wa Wanaume ndani ya Usharika wetu.Mkutano utakuwa mfupi sana.

 

5. NDOA ZA WASHARIKA

 

Kwa mara ya tatu tunatangaza ndoa  za tarehe 20/05/2017

 

SAA 8.00 MCHANA

Bw. Salim Athuman Kisuda  na     Bi. Sarah Laili Mussa

 

SAA 10.00 JIONI

Bw. Nzota Gideon Killango   na     Bi. Margareth Frank Mtui

 

Matangazo mengine ya Ndoa yamebandikwa kwenye ubao wa matangazo Karibu na duka letu la vitabu.

 

  1. Ibada za Nyumba kwa Nyumba
  • Upanga: Kwa Bwana na Bibi Happiness Nkya
  • Kinondoni:  Kwa Bwana na Bibi Edward Mkony
  •  
  • Kawe/Mikocheni/Mbezi Beach: Watatangaziana
  •  
  • Tabata: Watatangaziana
  •  
  • Mjini kati: Watatangaziana
  • Wazo/tegeta/Kunduchi/BahariBeach/Ununio: Kwa Bw. na Bibi Wilfred Moshi

 

Zamu: Zamu za wazee leo ni kundi la Pili.

 

Na huu ndio mwisho wa matangazo yetu, Mungu ayabariki.