PICHA: Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Umoja wa Wanaume | Azania Front Cathedral

Matukio mbalimbali katika picha kutoka katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Umoja wa Wanaume wa Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front uliofanyika siku ya Juampili, 19 Oktoba 2025 usharikani hapa. Mkutano huo uliongozwa na Mwenyekiti wa Umoja huo Kapteni John Joseph Mkony, na ulifunguliwa na Mchungaji Joseph Mlaki. Mkutano huu ni jukwaa muhimu linalowaleta pamoja wanaume wote wa usharika ili waweze kujadili mambo mbalimbali yanayohusu umoja huo na usharika wa ujumla.

Sikukuu ya Mikaeli na Watoto 2025 | Azania Front Cathedral

Siku ya Jumapili tarehe 28 Septemba 2025 katika Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front ilifanyika Sikukuu ya Mikaeli na Watoto; Sikukuu ambayo hufanyika kila mwaka kwa ajili ya kumkumbuka Malaika Mikeli na watakatifu wote pamoja na watoto. Ibada hii hufanyika kwa kuongozwa na watoto wakisaidiana na walimu wao pamoja na watumishi wengine wa usharika (parish workers).